• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

DK MAHIGA AZIKARIBISHA NCHI JIRANI MAONESHO YA UTALII YA KARIBU KUSINI

Posted on: October 3rd, 2017

DK MAHIGA AZIKARIBISHA NCHI JIRANI MAONESHO YA UTALII YA KARIBU KUSINI

Na. Frank Leonard

WAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk Augustine Mahiga amezikaribisha nchi jirani za Zambia, Malawi, Msumbuji na Kongo kushiriki maonesho ya Utalii ya Karibu Kusini yatakayokuwa yakifanyika kila mwaka mjini Iringa baada ya serikali kuutangza mkoa wa Iringa kuwa kitovu cha utalii cha mikoa ya Nyanda za Juu Kusini.


Aliyasema hayo jana wakati akifunga maonesho ya mwaka huu yaliyofanyika katika viwanja vya Kichangani mjini Iringa kati ya Septemba 29 na Oktoba 2.


“Ni maonesho yanayohusisha mikoa saba ya Nyanda za Juu Kusini ya Iringa, Njombe, Ruvuma, Mbeya, Songwe, Rukwa na Katavi. Muda umefika sasa tuzishirikishe nchi jirani na mikoa hii ili kuyafanya maonesho haya yawe ya kimataifa zaidi,” alisema.


Pamoja na kuzialika nchi hizo jirani, ameahidi kusambaza taarifa maalumu ya vivutio vya utalii vya kusini kwa mawakala mbalimbali wanaotangaza utalii wa Tanzania nje ya nchi.


Akifunga maonesho hayo Balozi Mahiga alisema; “Nimefurahishwa sana kushirikishwa katika maonesho hayo natarajia mwakani nitakuwa pamoja nanyi.”


Awali Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza alitoa takwimu zinazoonesha maonesho hayo yaliyofanyika kwa mara ya kwanza mwaka jana yakipata mafanikio zaidi mwaka huu.


Masenza alisema wakati mwaka 2016, washiriki katika maonesho hayo walikuwa 127 ambayo ni sawa na asilimia 42 ya washiriki 300 waliotarajiwa, mwaka huu washiriki wameongezeka hadi 435 sawa na asilimia 87 ya washiriki 500 waliotarajiwa.


Alisema kati ya washiriki hao, washiriki wanne ambao ni wajasiriamali wa viwanda vidogo walitoka nchini Kenya.


Alisema maonesho hayo yalijumuisha maeneo sita ambayo ni pamoja na maonesho ya bidhaa za wajasiriamali na watoa huduma za utalii, kongamano la utalii endelevu, usiku wa Utalii kusini, maonesho ya tamaduni na ngoma asilia, maonesho ya wanyama hai na ziara za kutembelea vivutio mbalimbali.


Katika risala yao iliyosomwa na Daimon Mwenda, wajasiriamali wenye viwanda vidogo walitaja changamoto wanazokumbuna nazo katika kuboresha shughuli zao za uzalishaji.


Changamoto hizo ni pamoja ukosefu wa baadhi ya malighafi ambazo hazizalishwi nchini, mlolongo wa kupata vibali na leseni za uanzishwaji viwanda, mitaji, ushindani na bidhaa toka nje na gharama za ununuzi wa mashine za kodi (EFDs).

=30=

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • ‎RC SERUKAMBA AITAKA TRA KUDHIBITI RISITI FEKI, KUHAMASISHA ELIMU YA KODI

    May 19, 2025
  • TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM MKOA WA IRINGA.

    May 18, 2025
  • UKAGUZI WA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA YA MUFINDI

    May 08, 2025
  • RC SERUKAMBA AHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA VIONGOZI NA WATUMISHI

    May 07, 2025
  • Tazama zote

Video

RC SERUKAMBA: WANANCHI PAWAGA FANYENI KAZI KWA BIDII.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2025, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.