• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

IRINGA NAFASI YA NNE MTIHANI WA DARASA LA SABA KITAIFA

Posted on: July 4th, 2018

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa

Mkoa wa Iringa umeshika nafasi ya nne kati ya mikoa 26 katika matokeo ya mtihani wa darasa la saba kwa mtihani uliofanyika mwaka 2017.

Kauli hiyo ilitolewa na afisa elimu taaluma Mkoa wa Iringa, Mwalimu Farida Mwasumilwe alipokuwa akiwasilisha taarifa ya maendeleo ya sekta ya elimu Mkoa wa Iringa katika kikao cha wadau wa elimu Wilaya ya Kilolo, kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri ya Wilaya ya Kilolo.

Mwalimu Mwasumilwe alisema kuwa Mkoa wa Iringa umekuwa ukifanya vizuri katika matokeo ya mtihani wa kumaliza darasa la saba kwa miaka kadhaa. “Kwa mtihani uliofanyika mwezi Septemba, 2017 Mkoa umeshika nafasi ya nne kati ya mikoa 26 ya Tanzania bara ukiwa na ufaulu wa asilimia 83.14 ambapo jumla ya wanafunzi 20,606 wamechaguliwa na kujiunga na kidato cha kwanza 2018, ukilinganisha na ufaulu wa mwaka 2015 ambapo mkoa ulikuwa nafasi ya 10 ukiwa na ufaulu wa asilimia 73.25” alisema Mwalimu Mwasumilwe. Ufaulu umekuwa ukiongezeka kwa halmashauri ya Manispaa ya Iringa na halmashauri ya Wilaya ya Kilolo, aliongeza.

Akiongelea, hali ya miundombinu na samani katika shule za msingi, afisa elimu taaluma mkoa alisema kuwa mkoa una vyumba vya madarasa 4,153, nyumba za walimu 2,203 matundu ya vyoo 7,283 na madawati 99,386. Mkoa umeendelea kuhakikisha miundombinu muhimu na samani vinapatikana katika shule ili kuboresha mazingira ya utoaji elimu, aliongeza.

Akiongelea mikakati ya kukabiliana na upungufu wa miundombinu, afisa elimu taaluma huyo alisema kuwa mkoa umeendelea kutenga fedha kupitia halmashauri zake kutoka katika mapato ya ndani, ruzuku ya serikali na kuwashirikisha wadau wa maendeleo kuchangia ujenzi wa miundombinu ya elimu katika shule za msingi.

Mkoa wa Iringa una jumla ya shule za msingi 499, zikiwa ni ongezeko la asilimia 3.1 mwaka 2018 ikilinganishwa na idadi ya shule 484 mwaka 2015.

=30=



Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • ‎RC SERUKAMBA AITAKA TRA KUDHIBITI RISITI FEKI, KUHAMASISHA ELIMU YA KODI

    May 19, 2025
  • TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM MKOA WA IRINGA.

    May 18, 2025
  • UKAGUZI WA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA YA MUFINDI

    May 08, 2025
  • RC SERUKAMBA AHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA VIONGOZI NA WATUMISHI

    May 07, 2025
  • Tazama zote

Video

RC SERUKAMBA: WANANCHI PAWAGA FANYENI KAZI KWA BIDII.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2025, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.