• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

JAMII YATAKIWA KUAMKA KUTETEA USAWA WA KIJINSIA

Posted on: November 24th, 2017

JAMII YATAKIWA KUAMKA KUTETEA USAWA WA KIJINSIA

Na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

Wanawake na watoto wameendelea kuwa wahanga wa vitendo vya ukatili wa kijinsia na kukabiliwa na mgawanyo usio sawa wa rasilimali na madaraka kutokana na mwamko mdogo wa jamii kuhusu usawa wa kijinsia.

Kauli hiyo ilitolewa na mkuu wa mkoa wa Iringa, Amina Masenza katika hotuba yake ya uzinduzi wa kampeni ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia, uliofanyika ngazi ya mkoa katika halmashauri ya wilaya ya Kilolo na kusomwa kwa niaba yake na mganga mkuu wa mkoa Dr Robert Salim.

Mkuu wa Mkoa alisema “katika mkoa wetu wa Iringa, vitendo vya ukatili wa kijinsia vimekuwa vikifanyika katika maeneo mbalimbali, wanawake na watoto wamekuwa ndiyo wahanga wakubwa. Kwa mfano, wanawake wameendelea kukabiliwa na mgawanyo usio sawa wa rasilimali na madaraka kati yao na wanaume, kukosekana kwa usawa kunakichangiwa na mfumo dume uliopo katika jamii, wanawake kunyanyaswa, kubaguliwa, kupigwa, kutelekezwa na watoto, kutokushirikishwa katika maamuzi hata yale yanayohusu maisha yao”. Aliongeza kuwa watoto pia wamekuwa wakinyimwa haki zao za msingi katika jamii.

Mkuu wa mkoa alisema kuwa kumekuwa na matukio ya watoto kubakwa na kulawitiwa, mimba za utotoni, kupigwa na kuterekezwa. ”Idadi ya watoto waliofanyiwa ukatili wa aina tofauti kwa kipindi cha kuanzia Julai 2016- hadi Oktoba, 2017 imefikia watoto 606. Watoto 306 wameripotiwa kufanyiwa ukatili wa kingono na watoto 300 ukatili mwingine kama kupigwa na kadharika. Inashangaza kuona kwamba idadi kubwa ya vitendo vya ukatili dhidi ya watoto vimekuwa vikifanywa majumbani, shuleni au njiani, ukatili huu umekuwa ukifanywa na watu au ndugu wa karibu wa familia husika” alisisitiza Mkuu wa Mkoa.

Mkuu wa Mkoa alisema kuwa kwa kipindi cha miaka miwili, wanawake 904 wamefanyiwa ukatili. Ukatili huo umewaathiri kiafya, kijamii, kisaikolojia na kiuchumi. Ukatili wa kijinsia umekuwa ukichangia kuongezeka kwa maambukizi ya virusi vya ukimwi na magonjwa mengine yatokanayo na ngono.

=30=





Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • ‎RC SERUKAMBA AITAKA TRA KUDHIBITI RISITI FEKI, KUHAMASISHA ELIMU YA KODI

    May 19, 2025
  • TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM MKOA WA IRINGA.

    May 18, 2025
  • UKAGUZI WA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA YA MUFINDI

    May 08, 2025
  • RC SERUKAMBA AHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA VIONGOZI NA WATUMISHI

    May 07, 2025
  • Tazama zote

Video

RC SERUKAMBA: WANANCHI PAWAGA FANYENI KAZI KWA BIDII.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2025, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.