• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

Katibu Tawala Mkoa Mh. Happiness Seneda Aongoza kikao cha kutangaza matokeo ya Darasa la Saba kwa wanaotarajia kuanza Kidato cha Kwanza mwaka 2020

Posted on: December 6th, 2019


Kikao hicho ambacho kimefanyika leo tarehe 06/12/2019 Mkoa Mkoani humo. Iringa ni kati ya  Mikoa iliyofanya vizuri katika mitihani ya Darasa la Saba kwa mwaka 2019 kati ya Mikoa 26 ya Tanzania Bara. Mkoa wa Iringa umekuwa katika nafasi ya tatu ngazi ya Taifa na kupata tuzo bora ya ufaulu.

‘Nawapongeza walimu na watendaji wote kwa kufanya vizuri katika usimamizi wa mitihani ya Darasa la Saba kwa mwaka huu 2019 na kupata nafasi hii ya tatu Kitaifa’. Ameyasema haya wakati wa kikao hicho Katibu Tawala wa Mkoa Bi. Happiness Seneda ambaye ndiye alikuwa Mwenyekiti wa kikao hicho.

Wanafunzi 25,325 walisajiliwa katika shule 496, sawa na 98.7% walifanya mitihani hiyo. Na 88.53% wamefaulu mitihani hiyo, ambapo ni ongezeko la 5.0% la 88.53% ukilinganisha na mwaka 2018 ambapo ilikuwa 83.06%.

Nawapongeza Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo kwa kuongeza ufaulu kwa 7.82% tofauti na mwaka jana. Ufaulu ni jambo muhimu sana kwetu, japo kuna changamoto za vyumba vya madarasa. Jumla ya watoto 3,480 hawajapangiwa kuanza kidato cha kwanza kutokana na ukosefu wa nyumba vya madarasa.

Halmashauri ya Manispaa ya Iringa na Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo zihakikishe wanashughulikia miundombinu ya vyumba vya madarasa ili watoto waanze shule mwezi Januari. Nawapongeza Halmashauri ya Mji Mafinga na Halmashauri ya Wilaya ya Mifindi kwa kutokuwa na upungufu wa vyumba vya madarasa.

Mwaka huu 2019 Mkoa haukukumbwa na tuhuma za udanganyifu, nawapongeza sana Kamati ya Mitihani kwa kusimamia vizuri.

Wito wang naomba usimamizi huu uendelee hadi ngazi ya Taifa.

Matokeo:

Waliofanya mtihani ni 24,784 (Wavulana 11,421 Wasichana 13,363), Waliofaulu kuanzia  100 – 250 ni 20,606 (Wavulana 9,513 Wasichana 11,093) sawa na 88.53% ukilinganisha na mwaka 2018 ambapo ilikuwa 83.4%, hivyo kwa mwaka huu 2019 matokeo yamepanda kwa 5.3%.

Imetolewa na Ofisi ya Habari Mkoa,

Humphrey Kisika.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • UKAGUZI WA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA YA MUFINDI

    May 08, 2025
  • RC SERUKAMBA AHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA VIONGOZI NA WATUMISHI

    May 07, 2025
  • MTIHANI MWEMA KIDATO CHA SITA

    May 04, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WAKAMILISHA ZIARA MKOA WA IRINGA NA KUKABIDHIWA MKOA WA NJOMBE

    May 03, 2025
  • Tazama zote

Video

RC SERUKAMBA: WANANCHI PAWAGA FANYENI KAZI KWA BIDII.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2025, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.