• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

KIWANDA CHA KARATASI MUFINDI CHATAKIWA KUZALISHA KARATASI NYEUPE

Posted on: September 9th, 2018

Serikali ya Mkoa wa Iringa imekiagiza kiwanda cha karatasi Mufindi (MPM) kuanza kuzalisha karatasi nyeupe ili kuongeza ajira kwa vijana na mapato ya Serikali.

Agizo hilo lilitolewa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe Ally Hapi alipokuwa akiongea na menejimenti ya kiwanda hicho baada ya kufanya ziara ya kukikagua jana.

Mhe Hapi alikiagiza kiwanda hicho kuanza kutengeneza karatasi nyeupe zinazotumika katika shajala mbalimbali kwenye ofisi na madaftari. Alisema kuwa wakati wa kukagua kiwanda hicho, amekuta mashine za kutengeneza karatasi nyeupe zimezimwa jambo linaloikosesha Serikali mapato. “Ndugu zangu, uzalishaji wa karatasi nyeupe katika kiwanda hiki utasaidia kuongeza ajira kwa vijana wetu, utapunguza gharama kubwa ya kununua karatasi nyeupe na kuongeza mapato ya Serikali. Hiki ni kiwanda kikubwa kilichokuwa kinategemewa na nchi.” alisema Mhe Hapi.

Mkuu wa Mkoa alisema kuwa eneo la kiwanda hicho lina uwekezaji mkubwa uliofanywa na Baba wa Taifa Mwl Julius Nyerere katika awamu ya kwanza ya utawala wake. “Serikali ya Mkoa inataka kubaini malengo ya Baba wa Taifa aliyokuwa nayo katika kiwanda hiki hadi mataifa mbalimbali yalikuwa yanakuja kujifunza katika kiwandani hapa. Nataka kujua masharti yaliyotolewa na Serikali wakati wa ubinafsishaji kama yametekelezwa na muwekezaji” alisema Mhe Hapi.

Vilevile, alishangazwa na reli ya TAZARA sehemu ya mchepuko wa kuingia kiwandani hapo kutokufanya kazi kwa muda mrefu. Alisema kuwa malengo ya Serikali kwa reli hiyo yalikuwa kurahisisha na kupunguza gharama za usafirishaji wa karatasi kutoka kiwandani hapo kuelekea maeneo mbalimbali ndani na nje ya nchi.

Kiwanda cha karatasi Mufindi kilibinafsishwa mwaka 2004 kikiwa na uzalishaji wa karatasi nyeupe na karatasi ngumu kikiwa na uwekezaji uliofanywa na Baba wa Taifa wa dola za kimerekani milioni 360.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • ‎RC SERUKAMBA AITAKA TRA KUDHIBITI RISITI FEKI, KUHAMASISHA ELIMU YA KODI

    May 19, 2025
  • TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM MKOA WA IRINGA.

    May 18, 2025
  • UKAGUZI WA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA YA MUFINDI

    May 08, 2025
  • RC SERUKAMBA AHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA VIONGOZI NA WATUMISHI

    May 07, 2025
  • Tazama zote

Video

RC SERUKAMBA: WANANCHI PAWAGA FANYENI KAZI KWA BIDII.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2025, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.