• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

LOCAL RADIO ZATAKIWA KUJIKITA VIJIJINI

Posted on: August 16th, 2017

Redio za ndani ya Mikoa zimetakiwa kujikita katika kutoa huduma ya habari za vijijini ili wananchi hao wanufaike na huduma hizo.

Kauli hiyo ilitolewa na mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Iringa ambaye ni Katibu Tawala Mkoa wa Iringa, Wamoja Ayubu alipokuwa akikagua banda la kituo cha redio cha Big Star katika uwanja wa maonesho ya Nanenane wa John Mwakangale mjini Mbeya.

Wamoja alisema kuwa redio za ndani zinawajabu wa kutoa huduma za habari zaidi vijijini. Aliongeza kuwa vituo vingi vya redio vipo katika makao makuu ya miji na masafa yake kuishia katika miji. “Local redio toeni huduma za habari za wananchi walio vijijini kwa sababu wanakosa fursa za kupata habari. Wananchi walio katika miji wana nafuu kwasababu redio nyingi zinapatikana mjini na vyombo vingine vya habari vinapatikana huko kama televisheni” alisisitiza Ayubu.

Aidha, alivitaka vituo vya redio kuwaalika viongozi wa umma katika redio kusikiliza kero za wananchi na kujibu hoja na maswali ya wananchi katika kuboresha utawala bora. Aliongeza kuwa vituo vya redio vitapotenga muda kwa ajili ya viongozi kusikiliza kero za wananchi kutasaidia katika utatuzi wa kero na kuwawezesha wananchi kuchapa kazi katika mazingira mazuri na rafiki. “Endeleeni kuhabarisha wananchi kwa sababu wananchi wanawategemea na kuwahitaji zaidi” alisisitiza Ayubu.  

Kituo cha redio cha Big Star kilianza kurusha matangazo yake mwaka 2015 mjini Mbeya katika masafa ya 106.3 MHz kwa sasa redio hiyo inasikika katika mikoa ya Mbeya na Songwe, na baadhi ya maeneo ya mikoa ya Rukwa, Katavi, Njombe, Iringa na Ruvuma.

Maonesho ya shughuli za wakalima Nanenane mwaka 2017 yanaongozwa na kauli mbiu isemayo, “zalisha kwa tija mazao na bidhaa za kilimo, mifugo na uvuvi kufikia uchumi wa kati”.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAAFISA ELIMU WAAGIZWA KUSIMAMIA MAENDELEO YA MICHEZO MASHULENI

    June 29, 2025
  • MASHINDANO YA UMITASHUMTA NA UMISSETA 2025 YACHAGIZA UCHUMI WA IRINGA.

    June 29, 2025
  • KARIBU MKOANI IRINGA

    June 28, 2025
  • RC SERUKAMBA AMESHIRIKI NA MAMIA YA WAOMBOLEZAJI KWENYE MAZISHI YA MDOGO WAKE NA WAZIRI WA NCHI OFISI YA WAZIRI MKUU MHE WILLIAM LUKUVI

    June 07, 2025
  • Tazama zote

Video

WASHIRIKI 10,000 KUTIKISA MASHINDANO YA UMITASHUMTA NA UMISSETA 2025 MKOANI IRINGA
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2025, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.