• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

MKOA WA IRINGA WAZINDUA MPANGO WA USAFI WA MAZINGIRA ENDELEVU

Posted on: September 26th, 2025

MKOA WA IRINGA WAZINDUA MPANGO WA USAFI WA MAZINGIRA ENDELEVU

Katika juhudi za kuhakikisha kila mwananchi anapata huduma bora na salama za maji na kuishi katika mazingira safi, Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Kheri James, leo Septemba 26, 2025, amezindua mpango mkakati wa uendelevu wa ubora wa usafi wa mazingira mkoani Iringa.

Uzinduzi huo umefanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa ambapo Mhe. James amebainisha kuwa mpango huo unalenga kuhakikisha kila mtu anapata huduma bora na salama za maji ifikapo mwaka 2030, sambamba na kuimarisha afya za wananchi na mazingira kwa ujumla.

Aidha, Mhe. James amewataka wakuu wa shule na viongozi wa taasisi mbalimbali kuhakikisha wanadumisha juhudi za kutunza na kuhifadhi mazingira kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vijavyo.

“Mazingira safi ni msingi wa afya na maendeleo ya jamii. Nawasihi viongozi wote kushirikiana kuhakikisha tunadumisha jitihada hizi kwa vizazi vya sasa na vijavyo,” alisema Mhe. James.

Mkuu wa Mkoa pia amewapongeza viongozi wa mkoa pamoja na wataalam wa sekta ya afya akisema mchango wao mkubwa ndio umewezesha kufikiwa kwa malengo ya awali katika kuboresha hali ya usafi na upatikanaji wa huduma za maji safi na salama.

Akizungumza na vyombo vya habari, Afisa Afya wa Mkoa wa Iringa, Bi. Khadija Haroun, alisema mpango huo utatekelezwa kuanzia mwaka 2025 hadi 2030. Alifafanua kuwa mkoa wa Iringa tayari umekamilisha hatua ya kuhakikisha kaya zote zinakuwa na vyoo bora, hatua iliyosaidia kufanikisha malengo ya awali katika usafi wa mazingira.

Kwa mujibu wa Bi. Haroun, utekelezaji wa mpango huo unatarajiwa kuongeza ushirikiano wa jamii, taasisi na serikali, ili kuimarisha afya na kulinda mazingira kwa maendeleo endelevu ya mkoa.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MKOA WA IRINGA WAZINDUA MPANGO WA USAFI WA MAZINGIRA ENDELEVU

    September 26, 2025
  • KIKAO CHA LISHE CHAONYESHA MAFANIKIO MKOANI IRINGA

    September 11, 2025
  • Dkt. MGIMBA AONGOZA TIMU KUKAGUA MIUNDOMBINU YA AFYA IRINGA

    August 21, 2025
  • DKT. SAMIA AIBADILISHA IRINGA KWA Bil. 7.5 ZA ELIMU

    August 05, 2025
  • Tazama zote

Video

MAENDELEO KWA SASA BILA MAWASILIANO HAYAWEZEKANI- RC KHERI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2025, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.