• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

RC HAPI AANZA ZIARA WILAYA YA KILOLO

Posted on: August 13th, 2018


Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe Ally Hapi ameanza ziara ya kutembelea Wilaya za Mkoa wa Iringa, akianza na Wilaya ya Kilolo.

Akiwa Wilayani Kilolo, alifanya kikao na Kamati ya Ulinzi na Usalama na kusisitiza umoja na mshikamano. Vilevile, aliitaka Kamati hiyo kuweka utaratibu wa kubadilishana taarifa kwa wakati ili ziwawezeshe kufanya maamuzi sahihi katika kazi zao.

Mkuu wa Mkoa alitembelea ofisi ya CCM Wilaya ya Kilolo na kufanya kikao na kamati ya siasa ya Wilaya hiyo. Aliomba ushirikiano katika kuijenga Iringa mpya. Aidha, aliomba umoja na ushirikiano kuendelea kudumishwa kwa mkuu we Wilaya, Mkurugenzi na wakuu wa idara katika kutekeleza Ilani ya CCM.

Mkuu wa Mkoa alifanya kikao na watumishi wa Wilaya ya Kilolo na kuwataka kuwa wamoja. "Natamani kujenga Iringa mpya yenye umoja, umoja baina ya viongozi na watumishi. Tunapanga pamoja na tunatekeleza pamoja. Msitangulize ubinafsi wenu bali tangulizeni umoja wenu" alisisitiza mhe Hapi.


Aidha, aliwataka watumishi kutambua kuwa vyeo vyao ni dhamana ambazo wamepewa kwa ajili ya kuwatumikia wananchi. "Kila mmoja lazima awaheshimu wananchi wa Kilolo. Tusiwajibu ovyo, wala kuwa na kiburi. Tuwasikilize na kuwahudumia. Wananchi hawa ndiyo walipa kodi na wanaotulipa mishahara" alisisitiza mhe Hapi.


Mkuu wa Mkoa alisisitiza uadilifu na kufanya kazi kwa haki na kuzingatia sheria. Alikemea vitendo vya rushwa na kusisitiza utunzaji wa siri za ofisi.

Mhe Hapi aliitaka halmashauri ya Wilaya ya Kilolo kujikita katika ukusanyaji mapato na kudhibiti matumizi yasiyo ya lazima ya fedha za serikali.


Katika kikao na wazee wa Wilaya ya Kilolo, Mkuu wa Mkoa aliwataarifu wazee hao kuwa alienda kujitambulisha kwao na kuomba ushirikiano wao katika kufikia malengo ya serikali. Aliwahakikishia wazee hao kuwa watendaji wa serikali wataendelea kutoa huduma nzuri kwa wananchi ili waendelee kuiunga mkono nakuiamini serikali yao. "Nimewaagiza watendaji kuwafuata wananchi huko mlipo na siyo nyie kuja kuwafuata watendaji walipo" alisisitiza mhe Hapi.

Katika mkutano wa hadhara, aliwahakikishia wananchi kuwa watendaji watawahudumia na kusikiliza kero zao na kuzipatia ufumbuzi kwa wakati. Aliwataarifu wananchi kuwa amewaagiza watendaji wa serikali kutoka ofisini na kuwafuata Wananchi katika maeneo yao na kutatua kero zao.

Mkuu wa mkoa yupo katika ziara yake ya wilaya kwa wilaya kwa lengo la kujitambulisha na kuelezea mwelekeo wa ujenzi wa Iringa mpya anayokusudia katika uongozi wake.

=30=

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • ‎RC SERUKAMBA AITAKA TRA KUDHIBITI RISITI FEKI, KUHAMASISHA ELIMU YA KODI

    May 19, 2025
  • TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM MKOA WA IRINGA.

    May 18, 2025
  • UKAGUZI WA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA YA MUFINDI

    May 08, 2025
  • RC SERUKAMBA AHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA VIONGOZI NA WATUMISHI

    May 07, 2025
  • Tazama zote

Video

RC SERUKAMBA: WANANCHI PAWAGA FANYENI KAZI KWA BIDII.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2025, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.