• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

RC HAPI AHOJI MATUMIZI YA FORCE ACCOUNT WILAYANI MUFINDI

Posted on: September 11th, 2018

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa-Iringa

Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe Ally Hapi amesikitishwa na matumizi ya ‘force account’ katika ujenzi wa nyumba ya walimu katika Kata ya Mapanda, Tarafa ya Kibengu wilayani Mufindi leo.

Mhe Hapi alisema kuwa baada ya kukagua mradi wa ujenzi wa nyumba moja ya walimu familia sita (6 in one) katika shule ya sekondari Ilogombe, hakuridhika na baadhi ya mambo katika ujenzi huo. “Utaratibu wa matumizi ya ‘force account’ hautekelezwi vizuri. Fedha zinaletwa ili wananchi wanufaike nazo. Nasikitika fundi hatoki kijiji hiki, wala kata hii, wala tarafa hii. Fundi anatoka Mgololo Kata ya Makungu Tarafa ya Kasanga. Hilo siyo lengo la serikali wala ‘force account’. Fundi katumia shilingi milioni 24, lengo ni fedha zibaki katika eneo mradi unapotekelezwa ili wananchi wanufaike nazo” alisema Mhe Hapi.

Mkuu wa Mkoa, aliwapongeza kwa ujenzi wa nyumba moja ya walimu familia sita katika shule ya sekondari Ilogombe na kushauri kuwa vyumba viwe vinajengwa vikubwa zaidi tofauti na vilivyojengwa. Aidha, aliwakumbusha wataalam kuwa siyo lazima fedha zinazoletwa kwa ajili ya ujenzi wa mradi ziishe, zinazobaki zitumike katika miradi mingine ya maendeleo. “Imejengeka tabia ya kuhakikisha fedha zote zinaisha bila kubaki hata kama mradi umekamilika na fedha kubaki, italazimishwa hapo ili fedha zote zionekane zimeisha” alisisitiza Mhe Hapi.

Mkuu wa Mkoa wa Iringa yupo katika siku yake ya tatu ya ziara ya Tarafa kwa Tarafa akiwa katika Tarafa ya Kibengu amezindua nyumba moja ya walimu ya familia sita katika shule ya sekondari Ilogombe, kukagua ujenzi wa bweni la wanafunzi na miundombinu ya shule ya sekondari Kihansi na kufanya mkutano na wananchi wa Tarafa ya Kibengu.  

=30=

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • UKAGUZI WA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA YA MUFINDI

    May 08, 2025
  • RC SERUKAMBA AHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA VIONGOZI NA WATUMISHI

    May 07, 2025
  • MTIHANI MWEMA KIDATO CHA SITA

    May 04, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WAKAMILISHA ZIARA MKOA WA IRINGA NA KUKABIDHIWA MKOA WA NJOMBE

    May 03, 2025
  • Tazama zote

Video

RC SERUKAMBA: WANANCHI PAWAGA FANYENI KAZI KWA BIDII.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2025, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.