• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

RC HAPI APONGEZA VIONGOZI WASTAAFU IRINGA

Posted on: August 6th, 2018


Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa

Viongozi wastaafu katika Mkoa wa Iringa wamepongezwa kwa mafanikio waliyoyapaka katika utumishi wao mkoani hapa.

Kauli hiyo ilitolewa na mkuu wa mkoa wa Iringa, Ally Hapi alipokuwa akiongea na kamati ya ulinzi na usalama na menejimenti ya mkoa wa Iringa katika hafla ya makabidhiano ya ofisi na mkuu wa mkoa mstaafu Amina Masenza katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya mkuu wa Mkoa.

Hapi alisema “tunawapongeza kwa mafanikio makubwa mliyoyapata katika uongozi wa mkoa wa Iringa. Pongezi kwa mkuu wa Mkoa na Katibu Tawala Mkoa kwa kazi nzuri mliyoifanya katika maendeleo ya mkoa wa Iringa. Pongezi kwa wakuu wa Wilaya kwa kazi nzuri, mlimpa mkuu wa Mkoa ushirikiano, umoja na upendo katika kutekeleza majukumu yake”.  

Akiongelea changamoto katika Mkoa, mkuu wa Mkoa alisema kuwa changamoto ndiyo sababu za kuwepo kwa viongozi. Hivyo, aliwataka viongozi wa serikali kujikita katika kutatua changamoto na kero za wananchi kwa wakati. Alisema kuwa utatuzi wa kero za wananchi kwa wakati unaondoa migogoro na misuguano na kuwapa wananchi muda wa kufanya kazi za maendeleo.

Hapi aliwaomba viongozi wastaafu kutoa ushirikiano kwa viongozi wapya katika kutekeleza majukumu yao. “Ninyi mnauelewa mkubwa katika mkoa huu, pale mnapoona nafasi ya kutushauri, kutupa taarifa msisite kufanya hivyo. Tunatarajia busara yenu na mawazo yenu katika kufikia mafanikio ya Mkoa wetu wa Iringa” alisema Hapi.

Awali mkuu wa mkoa mstaafu, Amina Masenza alisema kuwa hali ya ulinzi na usalama inaendelea kuimarika katika Mkoa wa Iringa kwa kushirikisha vyombo vyote vya ulinzi na usalama na wananchi kwa ujumla. Kutokana na hali ya usalama kuwa nzuri, wananchi wanaendelea kutekeleza majukumu yao vizuri, aliongeza. Hali ya siasa ni nzuri, na utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi ya CCM unaendelea vizuri.

=30=


Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • ‎RC SERUKAMBA AITAKA TRA KUDHIBITI RISITI FEKI, KUHAMASISHA ELIMU YA KODI

    May 19, 2025
  • TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM MKOA WA IRINGA.

    May 18, 2025
  • UKAGUZI WA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA YA MUFINDI

    May 08, 2025
  • RC SERUKAMBA AHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA VIONGOZI NA WATUMISHI

    May 07, 2025
  • Tazama zote

Video

RC SERUKAMBA: WANANCHI PAWAGA FANYENI KAZI KWA BIDII.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2025, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.