• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

RC Hapi awaonya wanaokopesha "fedha za moto"

Posted on: May 7th, 2020

Mkuu wa Mkoa Iringa Mheshimiwa Ally Hapi aongoza jopo la TAKUKURU kukabidhi magari ya wananchi walioporwa kwa misingi ya dhuluma tarehe Mei 07, 2020.

Mheshiwa Hapi amekabidhi magari hayo kwa wananchi ambao walikopa fedha katika taasisi (SACCOS) ambazo si halali na kusababisha wananchi kushindwa kulipa mikopo kwa kuwazidishia riba na hatimaye kuonekana mkopo haumaliziki na kupelekea kuporwa mali zao.

Akiongea na Wanahabari leo Mheshimiwa Hapi amesema, wananchi wanahitaji fedha kutoka Taasisi mbalimbali za kukopesha, lakini kuna watu wameibuka na kuvunja sheria za nchi na kukopesha bila kufuata sheria, na sehemu kubwa ya mikopo hii haieleweki riba zake zinakokotolewa vipi. Serikali imekuwa imepambana na jambo hili kwa muda mrefu sasa. Wapo wakopeshaji hadi wanachukua kadi za benki kutoka kwa watumishi waliokopa. Mtu anaweza kumaliza mkopo lakini anaambiwa bado deni halijaisha.Hivi karibuni kumekuwa na uhujumu uchumi kupitia vyama mbalimbali vya ushirika, mwanachama anakopa na hataki kurejesha mkopo.

Leo nasimama hapa kueleza wenzetu TAKUKURU walivyofanya kazi nzuri kuweza kuwabana na kurejesha mikopo na magari yaliyoporwa kwa wananchi ambao walikopa fedha za moto.  Magari hayo ni fuso lenye namba T 165 BLW na Toyota Serena (Noah) lenye namba T 311 DDF ambayo yaliporwa tangu mwaka 2017.

Mheshimiwa Hapi aliendelea kusema, ninawahakikishia wananchi kuwa sisi viongozi tuna dhamana kubwa ya kusaidia wananchi katika matatizo yao. Tumerejesha mali za awananchi ambazo zimeporwa kupitia minada feki, mikopo ya moto. Pia kiasi cha Shilingi 3.4 bilioni zimeokolewa kutoka kwa watu waliokopa kwenye  vyama mbalimbali vya ushirika na kushindwa kurejesha. Nawasihi wananchi kuwa makini katika fedha za moto.

Naye Mkuu wa TAKUKURU Iringa ameeliza kuwa wanaendelea na ufuatiliaji wa madeni katika operasheni ili kuweza kuokoa fedha zaidi na kufanya uchunguzi wa masuala mbalimbali.

Pia mwananchi Mwalimu mstaafu (Bi Hadija Mazola) aliyeporwa gari kwa kukopa kiasi cha shilingi milioni mbili na akaweza kulipa kiasi cha shilingi milioni nne, lakini baadaye wakamuambia anadaiwa kiashi cha shilingi milioni nane. Aliposhindwa kulipa deni hilo ndipo akaporwa gari hiyo.

Nao wananchi walioporwa magari hayo waliishukuru Serikali na kuwapongeza kwa kazi wanazofanya. Kwani hawakutegemea kama magari yao yangerejea.

Imetolewa na:

Ofisi ya Habari Mkoa.

 

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • ‎RC SERUKAMBA AITAKA TRA KUDHIBITI RISITI FEKI, KUHAMASISHA ELIMU YA KODI

    May 19, 2025
  • TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM MKOA WA IRINGA.

    May 18, 2025
  • UKAGUZI WA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA YA MUFINDI

    May 08, 2025
  • RC SERUKAMBA AHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA VIONGOZI NA WATUMISHI

    May 07, 2025
  • Tazama zote

Video

RC SERUKAMBA: WANANCHI PAWAGA FANYENI KAZI KWA BIDII.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2025, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.