• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

Wasichana Miaka 14 Kuchanjwa Dhidi ya Saratani ya Kizazi Iringa

Posted on: April 24th, 2018

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa

Wasichana wenye umri wa miaka 14 mkoani Iringa wametakiwa kujitokeza kwa wingi katika vituo vya kutolea huduma za chanjo ili kupata chanjo ya saratani ya mlango wa kizazi.

Rai hiyo ilitolewa na mkuu wa mkoa wa Iringa, Amina Masenza alipokuwa akizindua chanjo mpya ya saratani ya mlango wa kizazi mkoani Iringa iliyofanyika katika uwanja wa mashujaa mjini Mafinga jana.

Masenza alisema kuwa serikali imeanzisha chanjo mpya ya saratani ya mlango wa kizazi kwa wasichana wenye umri wa miaka 14 nchini. Alisema kuwa chanjo hiyo ina lenga kuwakinga wasichana hao dhidi ya ugonjwa wa saratani ya mlango wa kizazi.

“Serikali inawaomba wananchi wetu wawahimize walengwa wote kufika katika kituo cha kutolea huduma za chanjo na akina mama nao wajitokeze kwa wingi ili waweze kufanyiwa uchunguzi dhidi ya ugonjwa wa saratani. Kwa kufanya hivyo kutasaidia kuwakinga na magonjwa na vifo, hii itaiwezesha serikali kutumia fedha ambazo zingetumika kugharamia matibabu zitumike katika miradi mingine ya maendeleo” alisema Masenza.

Alisema kuwa, chanjo ni uwekezaji katika uchumi wa taifa, serikali inatoa chanjo bila malipo katika vituo vya serikali, binafsi na mashirika ya dini na yasiyo ya kiserikali.

Kwa kuwa chanjo ni uwekezaji katika uchumi wa Taifa, serikali hutoa chanjo hizi bila malipo katika vituo vyote vinavyotoa huduma za chanjo vikiwemo vya serikali, binafsi, mashirika ya dini na yasiyo ya kiserikali.

=30=

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • UKAGUZI WA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA YA MUFINDI

    May 08, 2025
  • RC SERUKAMBA AHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA VIONGOZI NA WATUMISHI

    May 07, 2025
  • MTIHANI MWEMA KIDATO CHA SITA

    May 04, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WAKAMILISHA ZIARA MKOA WA IRINGA NA KUKABIDHIWA MKOA WA NJOMBE

    May 03, 2025
  • Tazama zote

Video

RC SERUKAMBA: WANANCHI PAWAGA FANYENI KAZI KWA BIDII.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2025, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.