• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

WATANZANIA KUWAENZI MARIA NA CONSOLATA KWA KUPENDANA

Posted on: June 6th, 2018

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

Watanzania wametakiwa kuwaenzi mapacha walioungana Maria na Consolata Mwakikuti kwa kupendana, kusaidiana na kuvumiliana katika kutekeleza majukumu yao.

Kauli hiyo ilitolewa na Waziri wa elimu, sayansi na teknolojia Prof. Joyce Ndalichako alipoongoza mamia ya wananchi katika mazishi ya mapacha hao kwa niaba ya serikali mkoani Iringa.

Prof. Ndalichako alisema kuwa Maria na Consolata wameacha funzo kubwa kwa watanzania. Mapacha hawa waliishi kwa upendo, kuvumiliana na kushirikiana. Maria na Consolata ni mashujaa. “Watanzania tunatakiwa kuwaenzi mapacha hawa kudumisha upendo, kusaidiana na kushirikiana” alisema Prof. Ndalichako. Aliongeza kuwa somo kubwa waliloliachia taifa ni kujituma katika kazi. Alisema kuwa ulemavu siyo kikwazo katika kutekeleza majukumu, bali ni maumbile tu na kuitaka jamii kutokuwatenga watu wenye ulemavu katika kushiriki shughuli za kijamii na kielimu.

Wakati huohuo, mkuu wa mkoa wa Iringa, Amina Masenza alisema kuwa Maria na Consolata walijitambua, kujiamini na kujikubali. Aliitaka jamii kutokuwaficha watoto wenye ulemavu kwa sababu serikali ya Dkt John Magufuli ipo kwa ajili ya kuwahuhumia. “Serikali itashughulika na wote wanaoficha watoto wenye ulemavu” alisisitiza Masenza. Aidha, aliipongeza kamati ya maandalizi ya mazishi ya Maria na Consolata kwa kazi nzuri.

Maria na Consolata Mwakikuti walizaliwa wilayani Makete mkoani Njombe zaidi ya miaka 21 iliyopita na kupata elimu ya msingi wilayani makete, elimu ya sekondari walipata wilayani Kilolo na elimu ya juu katika chuo kikuu cha kikatoliki cha Ruaha mjini Iringa.

=30=




Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • ‎RC SERUKAMBA AITAKA TRA KUDHIBITI RISITI FEKI, KUHAMASISHA ELIMU YA KODI

    May 19, 2025
  • TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM MKOA WA IRINGA.

    May 18, 2025
  • UKAGUZI WA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA YA MUFINDI

    May 08, 2025
  • RC SERUKAMBA AHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA VIONGOZI NA WATUMISHI

    May 07, 2025
  • Tazama zote

Video

RC SERUKAMBA: WANANCHI PAWAGA FANYENI KAZI KWA BIDII.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2025, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.