• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

WATUMISHI WANAOSHIRIKI MCHEZO WA MPIRA WA MIGUU MKOANI IRINGA WATAKIWA KUCHEZA KWA NIDHAMU

Posted on: January 20th, 2018


WATUMISHI WANAOSHIRIKI MCHEZO WA MPIRA WA MIGUU MKOANI IRINGA WATAKIWA KUCHEZA KWA NIDHAMU

Na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

Watumishi wa taasisi mbalimbali mkoani Iringa wametakiwa kucheza kwa nidhamu na kuepuka ugomvi katika mashindano ya mpira wa miguu yanayoendelea mkoani Iringa.

Kauli hiyo ilitolewa na mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza katika hotuba yake ya ufunguzi wa mchezo wa mpira wa miguu kwa taasisi za mkoa wa Iringa iliyosomwa kwa niaba yake na mkuu wa Wilaya ya Iringa, Richard Kasesela katika uwanja wa chuo cha ualimu Kleruu kilichopo Manispaa ya Iringa leo.

Masenza aliwataka wachezaji hao kucheza kwa nidhamu na kuepuka kuchochea ugovi. Alisema kuwa mchezo wa mpira wa miguu ni burudani na unajenga urafiki hivyo, mashindano hayo yatumike kutoa burudani na kujenga urafiki miongoni mwa wanamichezo hao. Aliongeza kuwa mashindano hayo yatumike kujenga uzalendo kwa watumishi wa umma na watumishi wa taasisi zisizo za kiserikali mkoani Iringa. Aidha, aliwataka wanamichezo hao kutengeneza mtandao utakaowaunganisha kama wanamichezo na watumishi wa taasisi mbalimbali.

Katika salamu za afisa michezo Mkoa wa Iringa, Kenneth Komba kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi, alisema kuwa michezo hiyo ni wazo la mkuu wa Mkoa wa Iringa kutaka kuwaunganisha watumishi wa taasisi za Mkoa wa Iringa kupitia mchezo wa mpira wa miguu. Alisema kuwa hadi kufikia jana jumla ya taasisi 21 zilikuwa zimejitokeza kushiriki mashindano hayo.

Wakati huohuo, mechi ya ufunguzi, timu ya Timu ya RAS Iringa ilikubali kichapo cha magoli 5 bila kutoka TANROADS.

Mashindano ya mpira wa miguu kwa taasisi za Mkoa wa Iringa ni mashindanao ya kwanza ya aina yake kufanyika mkoani hapa yakikabiliwa na changamoto ya udhanimi.

=30=

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • ‎RC SERUKAMBA AITAKA TRA KUDHIBITI RISITI FEKI, KUHAMASISHA ELIMU YA KODI

    May 19, 2025
  • TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM MKOA WA IRINGA.

    May 18, 2025
  • UKAGUZI WA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA YA MUFINDI

    May 08, 2025
  • RC SERUKAMBA AHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA VIONGOZI NA WATUMISHI

    May 07, 2025
  • Tazama zote

Video

RC SERUKAMBA: WANANCHI PAWAGA FANYENI KAZI KWA BIDII.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2025, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.