Ikiwa ni kilele cha maadhimisho ya siku ya wafanyakazi Duniani Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mhe. Peter Serukamba amewataka wafanyakazi nchini kuanza utaratibu wa kujiwekea akiba kwa maisha yajayoAkizungumza katika maadhimisho hayo Mhe. Serukamba amewasisitiza Watanzania kwa kusema kuwa Dunia inapaswa kuiga kutoka kwa wafanyakazi wa Tanzania kwa kuiga na wao kuanza kujiwekea akiba katika maisha yajayo kwenye familiaPia ameongeza kwa kuwataka wafanyakazi hao kuwa na maadili katika utendaji wa kazi wawapo Ofisini na pindi wanapowahudumia wananchi.Sambamba na hayo amewataka wafanayakazi hao kuendeleza mapambano ya kupambana na ukatili wa kijinsia na kutokomeaza
Mkuu wa mkoa wa Iringa Mhe. Peter Serukamba ameshiriki katika uzinduzi wa jengo la upasuaji mkubwa la kituo cha Afya cha Wenda kilichopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Iringa kinachomilikiwa na kanisa Katoliki jimbo la Iringa.
Katika uzinduzi wa jengo hilo zipo baadhi ya changamoto ambazo kituo hicho wanakumbana nazo kubwa ikiwemo miundombinu mibovu ya barabara ya kufikia katika kituo hicho, ambapo Mhe. Serekamba amemuagiza Katibu Tawala wa Mkoa na Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo kukutana na Meneja wa TARURA kuhakikisha wanatengeneza Barabara hiyo.
Aidha amesema Serikali inaendelea kutambua mchango mkubwa unaofanywa na Taasisi za kidini katika kuhudumia jamii hivyo ameahidi kuwa Serikali itaendelea kushirikiana na Taasisi za kidini.
Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mhe. Peter Serukamba amemuagiza Katibu Tawala na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa kukutana na Meneja wa Wakala wa Barabara za Vijajini na Mijini TARURA kuzungumza nae kwaajili ya Ujenzi wa barabara iendayo katika kituo cha Afya cha wenda kinachomilikiwa na kanisa la Katoliki Jimbo la Iringa.
Hayo yamejiri wakati aliposhiriki katika uzinduzi wa jengo la upasuaji mkubwa lililopo katika kituo hicho.
Akitoa taarifa ya kituo hicho mganga mfawidhi wa kituo hicho Sister Sabina Mangi amesema ujenzi wa jengo hilo mpaka kukamilika kwake ni zaidi ya Millioni Mia sita zimetumika kukamilisha jengo hilo wakati ununizi wa vifaa umegharimu kiasi cha shilingi Milioni Mia Mbili Tisini na Tano, ambapo amesema jengo hilo limeleta ukombozi kwa akina mama kwani kwa sasa wanafanyiwa upasuaji wa dharura na upasuaji wa kawaida katika kituo hicho.
Pia ameongeza kwa kusema mbali na mafanikio hayo lakini wanakumbana na changamoto ya miundombinu mibovu ya barabara ambapo wameiomba serukali iweze kuwasaidi mita 900 za barabara
Akizungumza katika hafla hiyo Mhe. Serukamba amepongeza jitihada kubwa zinazofanywa na taasisi za kidini kwa kutoa huduma za kijamii huku akiahidi na kuagiza kwa watendaji kuhakikisha wanakaa na kujadili na TARURA namna watakavyoondoa changamoto ya barabara inayoelekea katika kituo hicho.
"Nitoe Maagizo kwa Katibu Tawala wa Mkoa, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa mumlete mtu wa TARURA aje aangalie aone tunafanya nini kuboresha barabara hii"
Nao baadhi ya wananchi wametoa shukrani nyingi sana kwa serikali na kanisa kwa kukiendeleza kituo hicho tangu kilipoanza mpaka sasa.
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga
Anuani ya Posta: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania
Simu: +255 262 702 715
Mobile:
Barua pepe: ras@iringa.go.tz
Hakimiliki ©2024, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.