Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mheshimiwa Abdallah Hamis Ulega(MB) amezindua Miradi Miwili ya Maendeleo na kuweka Jiwe la Msingi mradi mmoja na kukagua Mradi Mmoja wa maendeleo katika Halmashauri ya Mji Mafinga yenye thamani zaidi ya shilingi Bilioni 3.Akizungumza Kwenye Mkutano wa hadhara uliofanyika tarehe 18/9/2024 katika viwanja vya Kituo cha Afya Ifingo Mheshimiwa Ulega amesema amefarijika kuona maendeleo Makubwa ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo ambayo imepokea fedha kutoka Serikali Kuu, Halmashauri ya Mji Mafinga na kikubwa zaidi uchangiaji wa nguvu za wananchi katika utekelezaji wa Miradi hiyo.“ Nimeweka Jiwe la Msingi katika Jengo la Mama na Mtoto katika Zahanati ya Rungemba jengo ambalo lilianza ujenzi kwa kuibuliwa na wananchi kwa nguvu zao wenye thamani ya shilingi Milioni 40 na Halmashauri ime jenga kwa mapato yake ya ndani shilingi Milioni 77. Hili na jambo la kujifunza.”Nitafikisha salamu hizi kwa Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa wananchi wa Mafinga wanafanya kazi kwa ushirikiano mkubwa na wanatekeleza Miradi ya Maendeleo kwa juhudi zao na hivyo kuunga mkono juhudi za Mheshimiwa Rais na kusukuma mbele gurudumu la Maendeleo la Mji Mafinga.Miradi iliyotembelewa na Mheshimiwa Waziri wa Kilimo Mhe Abdallah Ulega (MB) ni;-Kuweka Jiwe la Msingi Ujenzi wa Jengo la Mama na Mtoto katika Zahanati ya Rungemba, Uzinduzi wa Shule Mpya ya Kata Mtaa wa Ndolezi Kata ya Boma ( SEQUIP), Kuzindua madarasa mawili katika Shule ya Msingi Kikombo na kutembelea ujenzi wa nyumba ya walimu(2 in 1) kupitia Mradi wa SEQUIPKatika Ziara hiyo Mbunge wa JimboLa Mafinga Mjini na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Cosato Chumi amekabidhi vitanda 6 katika Zahanati ya Rungemba kwaajili ya jengo la mama na mtoto kuunga mkono juhudi za Serikali na wananchi walioibua mradi huo
Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mhe. Peter Serukamba amempokea Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega, ambaye amewasili Mkoani Iringa Kwaajili ya ziara ya kukagua na kuzindua Miradi inayotekelezwa na Serikali ya awamu ya Sita, ambapo leo ameanza kuzindua miradi ya Halmashauri ya Manispaa ya Iringa
Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mhe. Peter Serukamba Septemba 12,2024 amefunga mafunzo ya Muujibu wa sheria katika kikosi cha Jeshi 841 KJ MafingaKabla ya kufunga Mafunzo hayo Mhe. Serukamba alipokelewa na Mwenyeji wake ambaye ndiye Mkuu wa kikosi Kanali Issa Chalamila na badae akagua gwaride
Hakimiliki ©2025, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.